Na Katherine Weber

WAKATI hapa nchini Waislamu wakianzisha mkakati wa kuhakikisha vyakula na baadhi ya vipodozi vinaandaliwa kwa kufuata miongozo ya imani ya Kiislamu kwa kuanzisha taasisi ijulikanayo kama ‘Halal’, mfanyabiashara wa Uturuki ameanzisha duka la ngono, kupitia mtandaoni,  ambalo pia litafuata utaratibu wa ‘Halal’


Wasichana wa Kiislamu waliovalia hijab wakipita mbele ya duka la kufundisha kujamiiana lililoko katika mji wa Berlin, nchini Ujeruman,  Julai 12, 2007


Pamoja na kuuza bidhaa nyingine, duka hilo pia litatumika kutoa ushauri kwa Waislamu, wa jinsi ya ‘kujamiiana kwa kufuata halal’, au kujamiiana kwa kufuata sheria za Kiislamu, yaani Sharia.


Mjasiriamali huyo Haluk Murat Demirel, 38 ameanzisha kinachoitwa “Halal Sex Shop” baada ya rafiki zake kumwambia kuwa wamekuwa wakihangaika kutafuta ushauri kuhusiana na kujamiiana kwa kufuata utaratibu wa Kiislamu lakini hawapati.


“Mitandao mingi inaonesha tu picha za ngono ambazo zinawachefua Waislamu. Mambo mengi ya maana katika eneo hilo la kujamiiana hayapatikani. Yale ambayo yako kwenye mitandao hayajathibitishwa na Waislamu,” Demirel aliwaambia waandishi wa habari.


 Mtandao wa Demirel unaelezea huduma unayoitoa ni salama na inaangukia katika sheria za Kiislamu. Ukiingia katika mtandao huo, watumiaji wanashauriwa kuchagua kubonyeza kidude kimoja kama ni wanawake, au ubonyeza kidude kingine kama ni wanaume, na wanaelekezwa kufuata kurasa kutegemea na jinsi zao. Vichwa vya habari katika tovuti hiyo ni pamoja na “Kujamiiana katika Uislamu”, “Maisha ya kujamiiana katika Uislamu”, na “Mapenzi ya kunyonyana kulingana na Uislamu.” 


Huduma au bidhaa katika tovuti hiyo zinapatikana kwa malipo ya dola za Marekani, fedha za Uturuki (liras) au euro, na kila bidhaa inayonunuliwa kupitia tovuti hiyo huambatanishwa na kijitabu kidogo chenye maelezo kuhusu kujamiiana kwa kufuata Uislamu.


Waanzilishi wa tovuti hiyo wameandika katika tovuti hiyo kuwa, ingawa watu wengi  wanadhani Uislamu uko kinyume na mambo ya kujamiiana, ukweli ni  kwamba dini hiyo “inakubaliana na kujamiiana katika mazingira yaliyokubalika, kakma vile kwa wanandoa.


Kwa mujibu wa vyombo vya habari, yapo maduka machache sana ‘yanayouza huduma kama hiyo’ nchini Uturuki, nchi ya Kiislamu lakini yenye katiba inayofuata mfumo wa kisekula. 


Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Tayyip Erdogan mara kwa mara amekuwa akikosolewa kwa kuachia hali hiyo; yeye amekuwa akipendekeza kuwa maduka hayo yaitwe ‘ maduka ya mapenzi’, pia amewashauri wanawake wawe wanazaa idadi maalum ya watoto, huku akizuia vikali utoaji mimba nchini humo.


Hapa nchini, wakati mvutano wa nani mwenye haki ya kuchinja ulipokuwa ukizidi kupamba moto, Waislamu walikuwa wakikamilisha kazi ya kusajili chombo kitakachokuwa na wajibu wa kuhakikisha kuwa vyakula na vipodozi vinaandaliwa kwa kufuata ‘Halal’.


Baadhi ya makampuni ya juisi na vyakula mbalimbali yameanza kufungisha bidhaa hizo kwa kutumia vifungashio vyenye nembo ya ‘Halal’ ili kuthibitisha kuwa vinafaa kutliwa au kutumiwa na Waislamu.

0 comments:

Post a Comment

 
Top