Na Agness Mayagila, Arusha

Maelfu ya wanawake na mabinti kutoka mikoa ya Arusha, Kilimanjaro, na maeneo  jirani wamemiminika katika uwanja wa sheikh Amri Abeid mjini Arusha ili kujumuika kwa pamoja kumkataa jini mahaba ambaye wamedai amewatesa wanawake wengi na hivyo kuleta shida katika ndoa zao.
 


Aidha wanawake wengi walimiminika na kujaza uwanja huo mpaka nje  kuonesha namna ambavyo wamechoka na mateso ya mwovu shetani ambapo walipata fursa ya kumwabudu Mungu na kuingia katika maombi ya mzigo ili kumpinga jini anayewatesa

Akifundisha  katika kusanyiko hilo la aina yake Jumamosi iliyopita, Mtumishi wa Mungu Jovin Msuya alisema  kuwa, maneno mengi,kelele na kutotimiza wajibu kwa wanawake  ni chanzo kikubwa cha wanawake wengi kuteswa na jini mahaba jambo ambalo limeleta uharibifu mkubwa katika ndoa za walio wengi na wengine kushindwa kuhimili na kuacha ndoa zao.

Jovin ambaye ni Meneja wa kituo cha redio ya Kikristo cha Safina FM kilichoandaa kusanyiko hilo, alisema kwamba wanawake wengi hawatimizi wajibu wao kwa waume zao na hivyo kutoa mianya ya adui kupenyeza tabia zake katikati yao na hivyo kusababisha faraka na magomvi katika ndoa zao

Alisema kwamba wakati umefika kwa wanawake kuamua kwa dhati kutimiza wajibu wao ndani ya ndoa zao ili kuziba nafasi ambazo adui anaweza  kuzitumia kuzipiga ndoa zao ambapo alibainisha kwamba wanawake wengi hawafanyi wajibuwao ipasavyo na ndio mwanya wa adui shetani


Akinukuu katika maandiko matakatifu kutoka Mithali  7:

11, alisema kuwa wanawake wana maneno mengi ambayo shetani    anayatumia kuyateka maisha yao na kuongeza kwamba wanawake wanabudi kulitambua hilo na kulizingatia ili Mungu aziponye ndoa zao

Mtumishi  Jovin alisema kwamba jini mahaba anapomwingia mtu ni lazima aisome tabia ya wanandoa na kujua yale wanayoyapenda ili awafanyewasiyafanye na kujifanya mshirika (mwili mmoja) kwa kusudi la kuwapata wanandoa kwa urahisi

Katika hatua nyingine aliwataka wanawake kufanya bidii kumwomba mungu ili kurejesha mioyo ya waume zao kwao ikiwa ni pamoja na kuziba mianya ya adui katika ndoa zao

'Wanawake ni lazima mzibe nafasi ambazo adui anazitumia kuwaingia,timizeni wajibu wenu kwa waume zenu,mnasema uchawi unatumika kuwakamata waume zenu someni neno mjua kuishi na waume zenu'alisema jovin


Aliongeza kwamba wanaume hawapendi maneno mengi na kelele za wanawake  ambazo alizitaja kuwa zinawafanya wanaume wengi kuchelewa kurudi majumbani na kuwaasa wanawake kujichunguza upya na kumwomba Mungu awasaidie

Alisema hakuna uchawi wa kumkamata mwanaue bali ni kutimiza yote ayatakayo,kwa wao kuwa wasafi waowenyewe,mazingira,mapishi bora na engine yaliyo wajibu wao na kwamba wataona mabadiriko kwa waume zao

Aidha, kongamano hilo liliongozwa na kichwa kisemacho “Ukweli kuhusu vita ya mwanamke” ambapo lilipambwa na waimbaji mbalimbali wa kike  wa nyimbo za injili.

Next
This is the most recent post.
Previous
Older Post

0 comments:

Post a Comment

 
Top